https://go.ad2upapp.com/afu.php?id=897810

KWA HABARI ZA KITAIFA KIMATAIFA MICHEZO MUZIKI BURUDANI NA AFYA KILA SIKU

Monday, October 10, 2016

Sasa ruksa simba na yanga kutumia uwanja wa uhuru kwa michezo yao

uwanja-wa-uhuru

Bodi ya ligi Tanzania imethibitisha timu za Simba na Yanga zitautumia uwanja wa Uhuru kwa mechi zao za nyumbani baada ya serikali kuzizuia kuutumia uwanja wa taifa kama uwanja wao wa nyumbani kwenye mechi zao za ligi kuu.
Mtendaji mkuu wa bodi ya ligi Boniface Wambura amesema, mechi ijayo ya Yanga wataanza kucheza kwenye uwanja huo dhidi ya Mtibwa mchezo unaotarajiwa kuchezwa Alhamisi October 13.
“Mechi zao watacheza kwenye uwanja wa Uhuru, kwahiyo mechi zao zote za nyumbani watakuwa wakitumia uwanja huo. Serikali ilizifungia kutumia uwanja wa taifa, uwanja wa Uhuru uko wazi wanaweza kuutumia wakati wowote,” anathibitisha Boniface Wambura.

Awali vilabu hivyo vilikuwa vinautumia uwanja huo kwa mechi zao za ligi kabla ya Simba kuulamimikia kuwa unawasababishia majeraha wachezaji wao na kuomba kurudishwa kwenye uwanja wa taifa.
Serikali ilichukua uamuzi wa kuufungia uwanja wa taifa kufatia vurugu za mashabiki zilizozuka kabla na wakati wa mchezo wa Yanga vs Simba uliochezwa October Mosi. Kabla ya mechi hiyo, mashabiki waling’oa mageti manne kabla ya mashabiki wa Simba kung’oa viti wakati mechi ikiendelea kwa madai klabu yao ilikuwa ikionewa katika mchezo huo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Propellerads

UNGANA NA SISI HAPO CHINI

Search This Blog

http://go.ad2upapp.com/afu.php?id=917347

Text Widget

Copyright © SAYARI 360 | Powered by Blogger

//]]>