Wakulima wawili wazungu nchini
Afrika kusini wanaolaumiwa kwa kumlazimisha mwanamme mwafrika kuingia
kwenye jeneza kwa kupitita shamba lao wamenyimwa dhamana na mahakama.
Mwezi
uliopita Theo Martins Jackson na Willem Oosthuizen, walifunguliwa
mashtaka ya kuteka nyara na kudhuluma kwa viwango vya kusababisha
madhara ya kimwili.Walikamatwa baada ya video moja ya dakika ishirini ambayo ilirekodiwa tarehe 17 mwezi Agosti kuanza kusambaa mitandaoni ikionyesha mwanamme mzungu akimlazimisha mwanamme mwafrika kuingia kwenye jeneza, akimtishia kumumwagia mafuta na kumchoma.
Taarifa zinasema kuwa mwendesha mashtaka alipinga wawili hao kuachuliwa kwa dhamana akidai kuwa muathiriwa Victor Mlotshwa ametishiwa maisha tangu akamatwe.
Jaji anayesikiliza kesi ametaja kitendo hicho kuwa cha kushangaza na cha kibaguzi na kuongeza kuwa si jambo la kushangaza kuwa ulimwengi ulishtushwa nacho.
0 comments:
Post a Comment