https://go.ad2upapp.com/afu.php?id=897810

KWA HABARI ZA KITAIFA KIMATAIFA MICHEZO MUZIKI BURUDANI NA AFYA KILA SIKU

Friday, November 11, 2016

Mshindi Wa Milioni Mia Moja Za Vodacom M-pawa Akabidhiwa Kitita Chache

Pichani ni Bi Paulina Kulwa (Kulia) akikabidhiwa hundi ya mfano wa Tsh Milioni 100 baada ya kuibuka mshindi katika promosheni ya Jiongeze na M-Pawa
Hapa kazi tu ni kaulimbiu inayohamasisha watu kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia fursa mbalimbali zilizopo, usemi huu umetimia kwa Mama Paulina Kulwa mkazi wa Mwanza baada ya kukabidhiwa kitita cha shilingi milioni mia moja kutoka kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya CBA.

Paulina alikabidhiwa hundi hiyo katika ofisi za Vodacom jijini mwanza na Meneja Masoko na huduma za Kifedha Vodacom Tanzania, Noel Mazoya na kusema lengo la kuanzisha huduma hii ni kuwasaidia Watanzania kuwa na utamaduni wa kuweka akiba.
Aidha, Bi Kulwa baada ya kukabidhiwa hundi alisema “Namshukuru Mungu na Vodacom kuanzisha huduma hii maana tayari imenifanya kuwa milionea na kuanzisha ajira kwa Watanzania wengine, lakini pia watoto wangu wanaenda shule na nina nyumba”

Naye Mkuu wa kitengo cha masoko Benki ya CBA, Solomon Kawishe alishukuru ushirikiano kati ya Benki yake na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania kwa kuleta neema kwa Watanzania. 
Share:

0 comments:

Post a Comment

Propellerads

UNGANA NA SISI HAPO CHINI

Search This Blog

http://go.ad2upapp.com/afu.php?id=917347

Text Widget

Copyright © SAYARI 360 | Powered by Blogger

//]]>