https://go.ad2upapp.com/afu.php?id=897810

KWA HABARI ZA KITAIFA KIMATAIFA MICHEZO MUZIKI BURUDANI NA AFYA KILA SIKU

Monday, October 10, 2016

Wasichana wa Tanzania kufanya mahojiano na Michelle Obama kesho




Michelle Obama
Michelle Obama 

Wasichana 25 wa Tanzania wanatarajiwa kufanya majadiliano ya moja kwa moja na mke wa Rais wa Marekani,  Michelle Obama wiki ijayo.
Wasichana hao ni miongoni mwa wasichana wa nchi tatu watakaoshiriki majadiliano hayo yenye lengo la kumuwezesha mtoto msichana katika masuala mbalimbali na upatikanaji wa fursa.
Majadiliano hayo ni tukio litakalofanywa na Shirika la Plan International Tanzania na yatafanyikia katika ubalozi wa Marekani, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Msichana Duniani tarehe 11 Oktoba, 2016.
Mkurugenzi Mkazi wa Plan International Tanzania Jorgen Haldorsen amesema nchi nyingine zitakazoshiriki katika majadiliano na mke wa Obama ni Peru na Cambodia.
Alisema katika kuadhimisha siku hiyo, wadau wataombwa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na kundi hilo na kupewa nafasi ya kujifunza, kuongoza, kuamua na kuishi ili kuonesha thamani ya mtoto wa kike na hata kwa kuwapa fursa sawa.
Alisema watoto wa kike wamekuwa wakishindwa kufikia malengo yao kutokana na vikwazo kuanzia katika jamii, ambapo pindi wakiaminiwa wanaweza kufanya mambo mbalimbali katika eneo la kisiasa, kiuchumi na hata kijamii.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Propellerads

UNGANA NA SISI HAPO CHINI

Search This Blog

http://go.ad2upapp.com/afu.php?id=917347

Text Widget

Copyright © SAYARI 360 | Powered by Blogger

//]]>