https://go.ad2upapp.com/afu.php?id=897810

KWA HABARI ZA KITAIFA KIMATAIFA MICHEZO MUZIKI BURUDANI NA AFYA KILA SIKU

Monday, October 10, 2016

Mwalimu Auawa.....Anyofolewa Kiganja cha Mkono wa Kulia


Mwalimu Israel Mlowasa (40) wa Shule ya Sekondari Nkuhungu katika Manispaa ya Dodoma, amekutwa ameuawa nyumbani kwake na kiganja chake cha mkono wa kulia kukatwa na kuondoka na wauaji hao.

Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi inasema kwamba mauaji hayo yamefanyika juzi maeneo ya Chang’ombe Extension katika Manispaa ya Dodoma.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Nkuhungu, Fidelis Kaishozi alisema mwalimu huyo alipotea tangu Oktoba 2, mwaka huu na taarifa kutolewa Polisi.

Imeelezwa kuwa maiti ya mwalimu huyo ilikutwa katika pagala la nyumba eneo la Nkuhungu.

Hakuna mtu aliyekamatwa kuhusu mauaji hayo, msako mkali unaendelea ili kubaini wahusika na mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Rufaa Dodoma kwa uchunguzi zaidi wa madaktari
Share:

0 comments:

Post a Comment

Propellerads

UNGANA NA SISI HAPO CHINI

Search This Blog

http://go.ad2upapp.com/afu.php?id=917347

Text Widget

Copyright © SAYARI 360 | Powered by Blogger

//]]>