https://go.ad2upapp.com/afu.php?id=897810

KWA HABARI ZA KITAIFA KIMATAIFA MICHEZO MUZIKI BURUDANI NA AFYA KILA SIKU

Sunday, October 23, 2016

Kichuya akabidhiwa tuzo Simba

 img_4604
Uongozi wa klabu ya Simba umemkabidhi Shiza Kichuya tuzo ya mchezaji bora wa mwezi September baada ya winga huyo kuisaidia klabu yake kupata pointi 12 katika mechi nne alizocheza mwezi huo, matokeo ambayo yameifanya Simba kuendelea kuongoza ligi.
Kichuya aliisadia Simba kwa kufunga magoli na kusaidia magoli mengine kufungwa. Alifunga mabao matatu katika mechi mbili kati ya nne alizocheza.
Umekuwa ni utamaduni wa Simba kutoa tuzo ya mchezi bora kila mwezi ambapo wachezaji hupigiwa kura na mashabiki wa timu hiyo.
Mbali na tuzo hiyo, Kichuya pia alitangazwa mchezaji bora wa mwezi kwa upande wa ligi kuu Tanzania bara.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Propellerads

UNGANA NA SISI HAPO CHINI

Search This Blog

http://go.ad2upapp.com/afu.php?id=917347

Text Widget

Copyright © SAYARI 360 | Powered by Blogger

//]]>