Friday, December 9, 2016
Thursday, December 8, 2016
Rais Magufuli kuandika historia miaka 55 ya Uhuru
RAIS John Magufuli leo anatarajiwa kuongoza Watanzania katika kilele cha maadhimisho ya Miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara, yatakayofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mara yake ya kwanza kushiriki sherehe hizo.
Wanaume 45 wadai kupigwa na wake zao
WANAUME 45 walio kwenye ndoa wilayani Nkasi katika Mkoa wa Rukwa wamevunja ukimya wakidai kupigwa na kutelekezwa na wenzi wao, imebainika.
Hayo yalibainishwa na Mkuu wa Polisi Dawati la Jinsia na Watoto wilayani Nkasi, Anna Kisima katika kikao kilichoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Plan International Tanzania kupitia mradi wake wa kuzuia ndoa za utotoni, kilichoketi jana mjini Namanyere.

